“WANANCHI TUPO TAYARI KUMUUA SIMBA” MUDATHIR YAHYA.

KIUNGO wa timu ya Yanga Mudathir Yahya amejigamba kwa kusema wananchi ni binadamu na kesho wanaenda kupambana na Simba hivyo wapo tayari kuhakikisha wanashinda vita ya kesho ili kuhakikisha wanatwaa ubingwa msimu huu.

“timu ya Simba ina kikosi kizuri ila sisi pia tuna timu nzuri sana ya kupata ushindi kesho, wao wanashambulia vizuri na sisi tunazuia vizuri hivyo mchezo utakua mzuri na tuko tayari kumuua Simba” alisema Mudathir.

Naye kocha msaidizi wa Yanga Cedric Kaze amesema kesho ni mechi ya kihistoria ambayo timu nzima imejiandaa kupata matokeo mazuri na wanayo furaha kubwa kuwa na mchezaji kama Fiston Mayele mwenye uwezo wa kubadilisha matokeo muda wowote.

“timu yetu nzima ipo tayari kwa mechi ya kesho kwani ni mechi kubwa na ya kihistoria ambayo ushindi wake utatupa mwanga kuelekea mbio za kutetea kombe letu, mchezaji kama Mayele tunaamini atakua nguzo kubwa kwetu kupata ushindi kwani ameleta tofauti kubwa katika kikosi chetu na kuwa mfano mzuri kwa wachezaji wengine kupambana ili kuinufaisha timu yetu” alisema Kaze.

Yanga inaingia katika mchezo huo siku chache baada ya kushinda mabao 5-0 dhidi ya Kagera Sugar na kuendelea kujiweka kileleni katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa na alama 68.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *