DAR ES SALAAM NI NYEKUNDU NA NYEUPE

TIMU ya simba imefanikiwa kushinda mchezo wa Ligi Kuu NBC dhidi ya Yanga kwa mabao 2-0 baada ya miaka mitatu tangu wafanye hivyo mwaka 2019.

Simba ikiwa mwenyeji ilifanikiwa kumaliza mchezo kipindi cha kwanza kwa mabao yaliyofungwa na Henock Inonga na Kibu Denis yaliyofanya timu hiyo kufikisha mabao 62 kwa msimu huu.

Mchezo huo ulishuhudia golikipa wa Simba Ally Salum akiibuka shujaa wa mchezo kwa kuokoa nafasi za hatari zilizotengenezwa na Yanga na kumfanya kumaliza mchezo wake wa pili mfululizo bila kuruhusu bao lolote katika Ligi Kuu NBC.

Matokeo hayo yanaifanya Simba kufufua matumaini ya kutwaa ubingwa wa NBC kwa kufikisha alama 63 na kuisogelea timu ya Yanga yenye alama 68 huku ikisalia michezo minne kabla ya kutamatika kwa Ligi hiyo.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *