VITA MPYA LIGI KUU NBC

MABAO matano aliyofunga Saido Ntibazonkiza katika ushindi wa mabao 6-1 iliyopata timu ya Simba dhidi ya Polisi Tanzania yameibua ushindani mpya katika kinyang’anyiro cha ufungaji bora wa Ligi Kuu msimu huu.

Mabao hayo yamemfanya Saido kufikisha (15) na kumkaribia Fiston Mayele wa Yanga mwenye mabao 16.

Saido amefikisha mabao hayo ikiwa ni baada ya kutumikia timu mbili tofauti za Geita Gold katika duru la kwanza na Simba katika duru la pili.

Ushindani huu unaibua shauku kubwa ya kushuhudia michezo ya mwisho kwa vinara hawa ambapo Mayele atacheza dhidi ya Tanzania Prisons huku Saido akicheza na Coastal Union ya Tanga.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *