TIMU ya Singida Big Stars ya Singida imeendelea kuizika timu ya Ruvu Shooting iliyokwisha kushuka daraja baada yankuifunga mabao 2-1.
Ruvu ni timu iliyoshinda michezo michache ya Ligi Kuu ya NBC (Mitano) ikiwa imefunga mabao machache zaidi (19) ikifanikiwa kupata alama 20.
Singida imeendelea kujihakikishia nafasi ya kushiriki mashindano ya kimataifa msimu ujao ikikusanya alama 54 katika nafasi ya nne kwenye msimamo.
Matokeo hayo yanaifanya Singida kuwa alama mbili nyuma ya timu ya Azam iliyoshinda mabao 2-0 dhidi ya Coastal Union ya Tanga kwenye uwanja wa Mkwakwani.
Mabao yaliyofungwa na Idris Mbombo na Prince Dube yameendela kuiweka Azam nafasi ya tatu huku Coastal ikisalia nafasi ya 10 ikiwa na alama 33.