IKITAMATIKA siku sita zilizopita Ligi Kuu ya NBC imeshuhudia jumla ya mabao 561 yakifungwa kwa timu zote 16 zilizoshiriki Ligi hiyo.
Timu ya Simba imeibuka kinara ikifunga jumla ya mabao 75 ikiizidi kwa mabao 14 timu ya Yanga inayoshika nafasi ya pili baada ya kufunga jumla ya mabao 61.
Ikiwa timu ya kwanza kufunga bao katika mashindano ya msimu huu uliomalizika kupitia kwa Ally Bilali Ruvu Shooting imefunga mabao 19 pekee ikiwa ni idadi ndogo zaidi.
Timu ya Polisi Tanzania ya Kilimanjaro itakayoshiriki Ligi ya Championship msimu ujao baada ya kushuka daraja na kuungana na Ruvu imefungwa mabao mengi (54) huku timu ya Simba ikimaliza msimu kwa kufungwa mabao machache (17).