SIMBA YANGURUMA MANUNGU.

TIMU ya Simba imeanza Ligi Kuu ya NBC kwa kishindo baada ya kuifunga Mtibwa Sugar mabao 4-2 kwenye uwanja wa Manungu, Morogoro.

Msimu uliopita Jean Baleke aliifunga Mtibwa mabao matatu na leo ameendeleza ubabe kwa timu hiyo baada ya kufunga bao moja huku mabao mengine yakifungwa na Fabrice Ngoma, Esomba Onana na Clatous Chama.

Mabao ya kufutia machozi ya Mtibwa yamefungwa na Matheo Anthony aliyecheza mchezo wake wa kwanza wa Ligi Kuu ya NBC kama mchezaji wa Mtibwa Sugar.

Simba imepata ushindi huo siku nne baada ya kutwaa Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga kwenye uwanja wa Mkwakwani, Tanga kwa ushindi wa mikwaju ya penati 3-1.

Ligi hiyo itaendelea tena Agosti 19 kwa michezo miwili itakayochezwa kati ya Ihefu na Kagera Sugar uwanja wa Highland Estates na Namungo dhidi ya KMC itakayochezwa uwanja wa Majaliwa, Lindi.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *