LIGI ya NBC Championship imeendelea Leo Septemba 10 kwa michezo minne kuchezwa kwenye mikoa mitatu tofauti.
Mchezo wa mapema saa 8:00 mchana ulizikutanisha TMA na Stand United katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha na kumalizika kwa suluhu.
Mchezo mwengine ulizikutanisha Mbuni na Biashara United saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha na kumalizika kwa sare ya bao moja.
KenGold wakiwa katika uwanja wao wa nyumbani Sokoine mkoani mbeya wakagawana alama na Transit Camp kwa sare ya bao moja.
FGA Talents imekuwa timu pekee kwa siku ya leo kuondoka na alama tatu baada ya kuwafunga Ruvu shooting mabao 2-1 kwenye uwanja wa Jamnhuri mkoani Morogoro.
Ligi hiyo itaendelea tena kesho Septemba 11 kwa mchezo mmoja kuchezwa Pamba wakiwaalika Cosmopolitan kwenye uwanja wa Nyamagana mkoani Mwanza.
Hongereni FGA kwa ushindi huo