LIGI Kuu ya NBC itaendelea leo kwa michezo miwili kwenye mikoa ya Shinyanga na Dodoma.
Wababe wawili wa ligi ya NBC Championship msimu uliopita JKT Tanzania na Mashujaa wanakutana kwa mara ya kwanza ndani ya Ligi Kuu ya NBC katika uwanja wa CCM Kambarage mkoani Shinyanga saa 10:00 alasiri.
JKT Tanzania imeshinda mchezo mmoja huku ikifungwa michezo miwili na kupata sare mchezo mmoja na Mashujaa ikianza vizuri msimu bila kufungwa mchezo na wala kuruhusu bao na ikishinda michezo miwili na kupata sare michezo miwili.
Dodoma Jiji watakuwa wenyeji wa Azam FC katika uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma saa 1:OO usiku katika mchezo wa pili leo.
Azam imeshinda michezo yote mitatu ya Ligi Kuu NBC msimu huu ikiwa na alama tisa katika nafasi ya tatu huku Dodoma ikishinda mchezo mmoja, sare moja na kufungwa moja ikiwa na alama nne huku ikishika nafasi ya saba kwenye msimamo.