WASHINDI TUZO ZA MWEZI SEPTEMBA LIGI KUU YA NBC.

KAMATI ya tuzo ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imemtangaza mchezaji wa timu ya KMC ya Dar Waziri Junior kuwa mchezaji bora wa Ligi Kuu ya NBC kwa mwezi Septemba akiwashinda Jean Baleke wa Simba na John Nakibinge wa Tabora United.

Waziri ameifungia timu yake mabao mawili na kuisaidia kushinda michezo miwili ya mwezi Septemba dhidi ya JKT Tanzania na Geita Gold.

Kamati hiyo pia imemtangaza kocha wa KMC Abdihamid Moalin kuwa kocha bora wa mwezi baada ya kushinda michezo yote miwili KMC waliyocheza kwa mwezi Septemba.

Moalin amewashinda Roberto Oliveira wa Simba na Abdallah Mohamed wa Mashujaa baada ya kukusanya alama sita na kupanda kutoka nafasi ya 14 mpaka ya tano kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

Aidha kamati imemtangaza meneja uwanja wa Azam Complex Amir Juma kuwa meneja bora wa uwanja kwa mwezi Septemba.

 

 

 

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *