SIMBA YAKAA KILELENI, SINGIDA IKITAMBA LIGI KUU NBC.

TIMU ya Simba imeshinda mchezo wa nne mfululizo wa Ligi Kuu ya NBC msimu huu na kukaa nafasi ya kwanza kwenye msimamo baada ya kuifunga Tanzania Prisons ya Mbeya mabao 3-1 kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya.

Mabao ya Clatous Chama, John Bocco na Saidi Ntibazonkiza yameifanya Prisons iliyokuwa ya Kwanza kupata bao kupitia kwa Edwin Balua kupoteza mchezo wa tatu msimu huu unaowaweka nafasi ya 16 kwenye msimamo wa ligi hiyo.

Singida Big Stars imepata ushindi wa kwanza msimu huu ikicheza uwanja wa Manungu, Morogoro ugenini baada ya kuifunga Mtibwa Sugar bao 1-0.

Bao la Singida limefungwa na Elvis Rupia na kuifanya Singida kufikisha alama tano na kupanda mpaka nafasi ya nane kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

Ligi hiyo itaendelea tena kesho kwa michezo miwili kati ya Tabora United na Dodoma Jiji saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora huku mchezo wa pili ukiwa Coastal Union dhidi ya Azam Fc kwenye uwanja wa Mkwakwani, Tanga saa 1:00 usiku.

One comment

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *