COASTAL, DODOMA HAZIKAMATIKI LIGI KUU YA NBC

 

LIGI Kuu ya NBC imeendelea Leo kwa Michezo miwili kuchezwa kwenye mikoa miwili tofauti.

Mchezo wa mapema saa 10:00 alasiri ulizikutanisha JKT Tanzania dhidi ya Coastal Union katika uwanja wa Azam Complex, Dar na kushuhudia Coastal Union akiibuka na Ushindi wa Bao moja lililofungwa na Maabad Maulid Dakika ya 87 .

Coastal Union imepanda hadi nafasi ya 6 katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikifikisha jumla alama 19.

Mchezo wa pili ulizikutanisha Dodoma Jiji dhidi ya Ihefu katika uwanja wa Jamhuri, Dodoma na kumalizika kwa Dodoma kuibuka na ushindi wa bao 1 lililofungwa na mchezaji Yasin Mgaza dakika 55 ya mchezo.

Ligi hiyo itaendelea tena kesho kwa mchezo nmoja kati ya Mtibwa Sugar na Mashujaa Saa 10:00 alasiri katika uwanja Manungu, Morogoro.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *