LIGI KUU ya NBC inaendelea leo kwa michezo mitatu katika mikoa mitatu tofauti baada ya kusimama kwa siku moja.
Mchezo wa kwanza utazikutanisha Tanzania Prisons dhidi ya Namungo katika uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya saa 8:00 Mchana.
Geita Gold watawaalika Singida FG katika uwanja wa Nyankumbu, Geita saa 10:00 alasiri.
Mchezo wa mwisho utapigwa saa 1:00 usiku Kagera Sugar dhidi ya Azam FC katika uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera.
Kagera anaingia kwenye mchezo huu akiwa na kumbukumbu ya kupoteza kwa mabao matatu dhidi ya Simba huku Azam akiifunga JKT Tanzania kwa mabao 2-1 katika uwanja wa Azam Complex.