AZAM, SINGIDA, SIMBA KIBARUANI LEO ROBO FAINALI KOMBE LA MAPINDUZI.

 

KOMBE la Mapinduzi hatua ya robo fainali inaendelea leo visiwani Zanzibar huku wawakilishi watatu wa Ligi Kuu ya NBC wakiingia vitani.

Mchezo wa mapema saa 10:15 utawakutanisha wawakilishi wawili wa Ligi Kuu ya NBC Azam wakiwakabili Singida FG.

Azam wamefika hatua ya robo fainali baada ya kuongoza kundi A wakiwa na Alama saba baada ya michezo mitatu huku Singida FG wakimaliza nafasi ya pili kundi B baada ya kujikusanyia alama sita kwenye michezo mitatu.

Mwakilishi mwengine wa Ligi Kuu ya NBC Simba watakuwa na kibarua dhidi ya Jamhuri saa 2:15 usiku.

Simba wamefika hatua hii ya robo fainali baada ya kuongoza kundi B wakiwa na alama Saba baada ya kucheza michezo mitatu huku Jamhuri wakiingia kama best looser baada ya kumaliza nafasi ya tatu kundi C.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *