KOMBE la Mapinduzi hatua ya robo fainali inaendelea leo visiwani Zanzibar huku wawakilishi watatu wa Ligi Kuu ya NBC wakiingia vitani.
Mchezo wa mapema saa 10:15 utawakutanisha wawakilishi wawili wa Ligi Kuu ya NBC Azam wakiwakabili Singida FG.
Azam wamefika hatua ya robo fainali baada ya kuongoza kundi A wakiwa na Alama saba baada ya michezo mitatu huku Singida FG wakimaliza nafasi ya pili kundi B baada ya kujikusanyia alama sita kwenye michezo mitatu.
Mwakilishi mwengine wa Ligi Kuu ya NBC Simba watakuwa na kibarua dhidi ya Jamhuri saa 2:15 usiku.
Simba wamefika hatua hii ya robo fainali baada ya kuongoza kundi B wakiwa na alama Saba baada ya kucheza michezo mitatu huku Jamhuri wakiingia kama best looser baada ya kumaliza nafasi ya tatu kundi C.