BIASHARA, FGA TALENTS, PAMBA ZAONDOKA NA ALAMA 3 NBC CHAMPIONSHIP IKIUNGURUMA.

 

LIGI ya NBC Championship imeendelea kuunguruma hii leo Januari 7 kwa michezo mitatu kupigwa.

Biashara United ya mkoani Mara imewaalika Mbuni ya Arusha katika uwanja wa Karume, Mara saa 8:00 mchana na kumalizika kwa Biashara kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.

Kwa ushindi huu Biashara United inapanda hadi nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi ya NBC Championship wakifikisha alama 33 baada ya michezo 16.

Saa 10:00 alasiri katika uwanja wa Mabatini mkoani Pwani Cosmopolitan wakawaalika Pamba na mchezo kutamatika kwa Cosmopolitan kukubali kichapo cha mabao 2-1.

Ruvu Shooting ikawa mwenyeji wa FGA Talents saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Jamhuri, Dodoma na kushuhudiwa Ruvu Shooting kukubali kichapo cha mabao 3-2.

Michezo ya leo imehitimisha mzunguko wa 16 wa Ligi ya NBC Champioship 2023/2024.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *