LIGI ya NBC Championship imeendelea kuunguruma hii leo Januari 7 kwa michezo mitatu kupigwa.
Biashara United ya mkoani Mara imewaalika Mbuni ya Arusha katika uwanja wa Karume, Mara saa 8:00 mchana na kumalizika kwa Biashara kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.
Kwa ushindi huu Biashara United inapanda hadi nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi ya NBC Championship wakifikisha alama 33 baada ya michezo 16.
Saa 10:00 alasiri katika uwanja wa Mabatini mkoani Pwani Cosmopolitan wakawaalika Pamba na mchezo kutamatika kwa Cosmopolitan kukubali kichapo cha mabao 2-1.
Ruvu Shooting ikawa mwenyeji wa FGA Talents saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Jamhuri, Dodoma na kushuhudiwa Ruvu Shooting kukubali kichapo cha mabao 3-2.
Michezo ya leo imehitimisha mzunguko wa 16 wa Ligi ya NBC Champioship 2023/2024.