SINGIDA FG, SIMBA ZATINGA NUSU FAINALI KOMBE LA MAPINDUZI.

 

HATUA ya robo fainali ya kombe la mapinduzi imemalizika leo kwa michezo miwili kupigwa.

Robo fainaili ya kwanza kwa leo ilizikutanisha Azam na Singida FG saa 10:15 alasiri kwenye uwanja wa New Amaan Complex na kumalizika kwa Azam kukubali kichapo cha mabao 2-1.

Saa 2:15 usiku Simba ikawakabili Jamhuri na kumalizika kwa Simba kuibuka na ushindi wa bao 1-0 bao pekee la Simba likifungwa na Jean Baleke dakika ya 45+2.

Baada ya matokeo haya Simba na Singida FG watakutana kwenye hatua ya nusu fainali ya pili Jumatano saa 2:15 usiku.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *