HATUA ya robo fainali ya kombe la mapinduzi imemalizika leo kwa michezo miwili kupigwa.
Robo fainaili ya kwanza kwa leo ilizikutanisha Azam na Singida FG saa 10:15 alasiri kwenye uwanja wa New Amaan Complex na kumalizika kwa Azam kukubali kichapo cha mabao 2-1.
Saa 2:15 usiku Simba ikawakabili Jamhuri na kumalizika kwa Simba kuibuka na ushindi wa bao 1-0 bao pekee la Simba likifungwa na Jean Baleke dakika ya 45+2.
Baada ya matokeo haya Simba na Singida FG watakutana kwenye hatua ya nusu fainali ya pili Jumatano saa 2:15 usiku.