KEN GOLD TIMU KINARA UFUNGAJI WA MABAO NBC CHAMPIONSHIP.

 

TAYARI mizunguko 16 ya Ligi ya NBC Championship imechezwa na kushudia jumla ya mabao 286 yakifungwa.

Ken Gold ndiyo timu inayoongoza kwa ufungaji wa mabao ikifunga jumla ya mabao 29 katika michezo 16 waliyocheza.

Biashara United ndiyo inafuatia kwa ufungaji wa mabao ikifunga jumla ya mabao 28 kwenye michezo 16, Pamba wanafuata wakiwa na mabao 24 kwenye michezo 16.

Mbeya Kwanza na Mbuni zimefunga jumla ya mabao 23 kwenye michezo yao 16 zikitofautiana kwenye mabao ya kufungwa huku Mbeya kwanza ikifungwa mabao 15 na Mbuni ikifungwa 16.

Ruvu Shooting ndiyo timu iliyofunga mabao machache zaidi kuliko timu nyengine yeyote ikifunga mabao sita pekee.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *