Mzunguko wa 18 wa Ligi ya NBC Championship unaanza leo Januari 19 kwa michezo miwili kuchezwa kwenye mikoa miwili tofauti.
Mkoani Kilimanjaro Polisi Tanzania watawaalika Green Warriors saa 8:00 mchana kwenye uwanja wa Ushirika.
Saa 10:00 alasiri FGA Talents itakuwa mwenyeji wa Transit Camp kwenye uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro.
FGA Talents na Transit Camp zinapambana kujinasua kutoka nafasi za mwisho kwenye msimamo ambapo FGA Talents imekusanya alama 15 kwenye michezo 17 ikiwa kwenye nafasi ya 12 huku Transit Camp ikikusanya alama 14 kwenye michezo 17 ikiwa na nafasi ya 14.