NBC CHAMPIONSHIP HAKUNA MBABE LEO.

 

MICHEZO miwili ya mzunguko wa 18 ya Ligi ya NBC Championship imechezwa leo na michezo yote kumalizika kwa sare.

Mchezo wa kwanza ulizikutanisha Polisi Tanzania dhidi ya Green Warriors saa 8:00 mchana kwenye uwanja wa ushirika, Kilimanjaro na kumalizika kwa suluhu.

Saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro FGA Talents ikaikaribisha Transit Camp na kumalizika kwa sare ya mabao 2-2 .

Ligi hiyo itaendelea tena kesho kwa michezo mitatu kupigwa Mbuni itawakabili Pan African, Pamba dhidi ya Stand United na Mbeya City dhidi ya Mbeya Kwanza.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *