MECHI zote za Ligi ya NBC Championship sasa zitarushwa mubashara na mdhamini mwenye haki ya matangazo TV3.
TV 3 ambayo inapatikana kwenye chaneli namba 197 (dish) na 137 (antena) kwenye king’amuzi cha Startimes, awali ilikuwa ikirusha baadhi ya michezo lakini baada ya maboresho ya ratiba sasa michezo yote kuonekana mubashara kupitia chaneli hiyo.
Hii ni hatua kubwa kwa Ligi ya NBC Championship kwani vipaji lukuki vilivyopo huku vitakuwa na nafasi ya kuonekana kwa ukubwa zaidi ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.