TIMU ya Bishara United ya Mara imeiduwaza Pamba ya Mwanza baada ya kuifunga bao 1-0 kwenye mchezo uliopigwa uwanja wa Mwadui, Shinyanga.
Pamba iliyokuwa mwenyeji wa mchezo huo imeruhusu bao la dakika ya 87 lililofungwa na Ramadhan Kipalamoto na kuifanya timu hiyo kushuka kutoka nafasi ya pili mpaka ya tatu na kuipisha Biashara iliyokaa nafasi ya pili kwa tofauti ya mabao ya kufunga.
Mkoani Kilimanjaro timu ya Polisi Tanzania imeshindwa kutamba baada ya kulazishwa sare ya bao moja dhidi ya timu ya Transit Camp ya mkoani Dar es Salaam.
Polisi inakwea hadi nafasi ya nane ikiwa na alama 26 huku Transit ikisalia nafasi ya 13 baada ya kufikisha alama 16.
Ken Gold ya Mbeya inaendelea kushika nafasi ya kwanza ikiwa na alama 43 huku Ruvu Shooting ya Pwani ikisalia nafasi ya 16 na alama tatu ikiwa haijashinda mchezo wowote msimu huu.