MBEYA, ARUSHA NBC CHAMPIONSHIP ‘KINAWAKA’ LEO.

 

MICHEZO miwili ya Ligi ya NBC Championship inachezwa leo kwenye mikoa ya Mbeya na Arusha katika muendelezo wa mzunguko wa 19.

Mkoani Mbeya KenGold vinara wa NBC Championship itawakabili Mbeya Kwanza inayoshika nafasi ya tano kwenye msimamo saa 8:00 mchana kwenye uwanja wa Sokoine.

Mkoani Arusha TMA inayoshika nafasi ya sita na alama 34 itakuwa mwenyeji wa Pan Africans inayoshika nafasi ya 14 ikiwa na alama 15 katika mchezo utakaochezwa saa 10 alasiri kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Michezo yote miwili itakuwa mubashara kwenye chaneli ya TV3 inayopatikana kwenye king’amuzi cha Startimes.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *