BAADA ya kusimama kwa takribani siku 40 kupisha mashindano ya Mataifa ya Afrika yanayoendelea nchini Ivory Coast Ligi Kuu ya NBC inarejea tena Februari 2.
Ligi hiyo itarejea kwa mchezo mmoja utakaopigwa saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera kati ya Kagera Sugar na Yanga.
Ligi hiyo namba sita kwa ubora Afrika inarejea baada ya timu ya taifa ya Tanzania kushindwa kufuzu kwenye hatua ya 16 bora na kutolewa kwenye mashindano ya Mataifa ya Afrika.
Ni ‘Mastaa’ watatu pekee waliosalia kwenye mashindano hayo hadi sasa ambao ni Henock Inonga wa timu ya Simba, Stephane Aziz Ki wa Yanga na Djigui Diarra wa Yanga hivyo kuruhusu ligi hiyo kuendelea kwa mujibu wa kanuni.