‘STAA’ YUPI WA LIGI KUU YA NBC KUMFUATA INONGA ROBO FAINALI LEO ?

KOMBE la Mataifa ya Afrika linaendelea nchini Ivory Coast huku ‘Mastaa’ watatu wa Ligi Kuu ya NBC wakisalia hadi sasa kwenye mashindano hayo.

Mashindano hayo yanaendelea leo huku wachezaji wawili wa Yanga Djigui Diarra anaekipiga timu ya taifa ya Mali na Stephane Aziz Ki wa Burkina Faso wakikutana leo kila mmoja akitafuta nafasi ya kucheza robo fainali.

Tayari ‘staa’ mmoja wa Ligi Kuu ya NBC Henock Inonga anaecheza timu ya Simba ameshafuzu hatua ya robo fainali kwenye mashindano yake na timu ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo baada ya kuitoa timu ya Misri.

Mshindi wa mchezo wa leo kati ya Diarra na Ki Aziz ndiye atasalia kwenye mashindano hayo na atakayepoteza atarejea nchini kuitumikia timu yake kwenye michezo ya Ligi Kuu ya NBC inayotarajiwa kurejea Februari 2 kwa mchezo kati ya Kagera Sugar dhidi ya Yanga.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *