WAWAKILISHI wawili wa Ligi Kuu ya NBC Simba na Yanga wameipaisha Tanzania katika historia ya kuwa nchi pekee Afrika iliyoingiza timu mbili hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu wa 2023/2024.
Yanga imeingia hatua ya robo fainali baada ya kujikusanyia alama nane kwenye michezo sita ikishinda michezo miwili ikipata sare kwenye michezo miwili na kufungwa michezo miwili huku Simba ikiingia hatua hii na alama tisa kwenye michezo sita ikishinda miwili ikipata sare michezo mitatu na kufungwa mchezo mmoja pekee.
Yanga inatarajiwa kukutana na Mamelodi Sundowns, Petro de Luanda au Asec Mimosas huku Simba ikitarajiwa kukutana na Al Ahly, Petro de Luanda au Mamelodi Sundowns.
Hatua ya robo fainali itachezwa Kati ya Machi 29-31 kwa timu zote mbili kuanzia kwenye uwanja wa Nyumbani Benjamin Mkapa.