KENGOLD, BIASHARA VINARA WA USHINDI NBC CHAMPIONSHIP.

 

TAYARI mizunguko 22 ya Ligi ya NBC Championship sawa na michezo 176 imeshachezwa na Kushuhudiwa jumla ya mabao 401 yakifungwa.

KenGold na Biashara United ndiyo timu zinazoongoza kwa kushinda michezo mingi kwenye Ligi ya NBC Championship zikifanya hivyo mara 15 kila mmoja huku KenGold ikifunga mabao 37 na kuruhusu mabao 12 na kufikisha alama 50 kileleni mwa msimamo wa Ligi hiyo wakati Biashara ikifunga mabao 38 na kufungwa mabao 14 ikiwa na alama 49 katika nafasi ya pili kwenye msimamo.

Pamba na Mbeya Kwanza zinafuatia zikishinda michezo 14 kila mmojahuku Pamba ikishika nafasi ya tatu kwenye msimamo ikiwa na alama 47 ikifunga mabao 35 na kuruhusu 12 wakati Mbeya Kwanza ikishika nafasi ya nne kwenye msimamo ikiwa na alama 45 ikifunga mabao 35 na kuruhusu mabao 22.

Ruvu Shooting imeshinda mchezo mmoja pekee kwenye michezo 22 waliyocheza hadi hivi sasa wakifunga mabao 11 na kuruhusu 43 ikishika nafasi ya mwisho kwenye msimamo.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *