MZUNGUKO wa 23 wa Ligi ya NBC Championship umemalizika na kushuhudiwa jumla ya mabao 15 yakifungwa kwenye michezo 8.
kenGold inaendelea kusalia kileleni mwa msimamo wa Ligi hiyo ikıwa na alama 53 tofauti ya alama nne na timu ya Biashara United huku kila timu ikisalia na michezo saba.
Biashara United inashika nafasi ya pili ikiwa na alama 49 ikifuatiwa na Pamba yenye alama 48 huku nafasi ya nne ikishikiliwa na Mbeya Kwanza yenye alama 46.
Ruvu Shooting inaendelea kusota nafasi ya mwisho kwenye msimamo licha ya ushindi wake iliyoupata dhidi ya Copco ikiwa na alama 11 kwenye michezo 23.