HAWA HAPA WAKALI WA MECHI ZA NYUMBANI NBC CHAMPIONSHIP.

 

JUMLA ya michezo 184 ya Ligi ya NBC Championship imechezwa kwenye viwanja mbalimbali kwenye mikoa 11 tofauti ikihusisha michezo ya nyumbani na ugenini kwa kila timu shiriki.

Biashara United inaongoza msimamo kwa timu zilizoshinda mechi nyingi nyumbani ikifanya hivyo mara 10 kwenye michezo 12 iliyocheza kwenye uwanja wake wa nyumbani Karume mkoani Mara.

Mbeya Kwanza, Mbuni na Mbeya City zinafuata kila timu ikishinda michezo nane zikitofautiana kwenye michezo ya kucheza ambayo Mbeya kwanza imecheza michezo 10, Mbuni ikicheza 11 na Mbeya City ikicheza 12.

Ruvu Shooting ndiyo timu iliyoshinda michezo michache zaidi nyumbani ikishinda mchezo mmoja pekee.

One comment

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *