ISAMUHYO, KAITABA HAKUNA MBABE LIGI KUU YA NBC.

 

LIGI KUU ya NBC imeendelea leo Machi 13 kwa michezo miwili kuchezwa kwenye viwanja viwili tofauti.

Mchezo wa mapema saa 10:00 alasiri ulizikutanisha JKT Tanzania dhidi ya Tanzania Prisons na kumalizika kwa sare ya bao 1.

Bao la JKT Tanzania lilifungwa dakika ya 40 na Daniel Lyanga huku lile la Tanzania Prisons likifungwa na Samson Mbangula dakika ya 46 ya mchezo.

Kwa matokeo hayo JKT Tanzania inafikisha alama 20 ikiendelea kusalia nafasi ya 15 kwenye msimamo huku Tanzania Prisons ikifikisha alama 28 ikipanda hadi nafasi ya nne.

Mchezo wa mwisho ulizikutanisha Kagera Sugar dhidi ya Mtibwa Sugar saa 1:00 usiku kwenye uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera na kumalizika kwa suluhu, kwa matokeo haya Kagera inasogea hadi nafasi ya saba ikifikisha alama 24 huku Mtibwa Sugar ikiendelea kusalia nafasi ya mwisho kwenye msimamo.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *