LIGI Kuu ya NBC inaendelea leo Machi 11 kwa mchezo mmoja kuchezwa Kati ya timu ya Yanga na Ihefu kwenye uwanja wa Azam Complex mkoani Dar es salaam.
Yanga inaingia kwenye mchezo Huu ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza kwenye mchezo wa mwisho timu hizi zilipokutana msimu huu kwa mabao 2-1 kwenye uwanja wa Highland Estates mkoani Mbeya.
Ihefu ndiyo timu pekee iliyoifunga Yanga kwenye Ligi Kuu ya NBC msimu huu huku Yanga ikiwa haijapoteza mchezo wowote mpaka sasa baada ya kipigo hicho.
Yanga inashika nafasi ya kwanza kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa na alama 46 baada ya michezo 17 huku Ihefu ikiwa nafasi ya nane na alama 23 baada ya kucheza michezo 19.