AZİZ KI, FEITOTO WAKALI WA MABAO LIGI KUU YA NBC.

 

LIGI Kuu ya NBC imesimama kwa muda kupisha kalenda ya FIFA ya michezo ya kimataifa ya kirafiki kwa timu za taifa ambapo Tanzania Itacheza michezo miwili ya kirafiki dhidi ya Bulgaria na Mongolia.

Hadi Ligi hiyo inasimama jumla ya mabao 364 yamefungwa huku Yanga ikiwa ndiyo timu iliyofunga mabao mengi zaidi (49).

Stephane Ki Aziz wa Yanga na Feisal Salum wa Azam ndiyo wanaoongoza kwa upachikaji wa mabao kila mmoja akifunga mabao 13 yakiwemo mabao matatu “Hat trick” kwenye mchezo mmoja, Ki Aziz akifunga dhidi ya Azam na Feisal Salum akifunga dhidi ya Tabora United.

Waziri Junior wa KMC anafuatia akifunga mabao 11 kwenye mabao 23 ya timu yake msimu huu yakiwemo mabao matatu “hat trick” dhidi ya Tabora United.

Maxi Nzengeli wa Yanga anakamilisha idadi ya wakali wanne wa juu kwenye upachikaji mabao akifunga mabao 9.

Kagera Sugar ndiyo timu iliyofunga mabao machache zaidi kwenye Ligi Kuu ya NBC ikifunga mabao 13 kwenye michezo 21.

2 comments

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *