KIPRE JR KINARA WA PASI ZA MABAO LIGI KUU YA NBC.

 

JUMLA ya mabao 364 yameshafungwa hadi hivi sasa kwenye Ligi Kuu ya NBC huku jumla ya wachezaji 137 wakihusika kwenye kuyatengeneza mabao hayo.

Kipre JR ndiye kinara wa kutoa pasi za mabao akifanya hivyo mara nane kwenye mabao 47 ya Azam FC msimu huu.

Kouassi Yao na Stephane Aziz Ki wanafuatia kila mmoja akitoa pasi saba za mabao na kuwa na jumla ya pasi 14 za mabao kwenye mabao 49 ya Yanga msimu huu.

Clatous Chama wa Simba, Feisal Salum wa Azam, Impiri Mbombo wa Tabora, Rahimu Shomari na Awesu Awesu wa KMC wanafuatia kila mmoja akitoa pasi 5 za mabao.

One comment

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *