MSIMU wa 2023/2024 Ligi ya NBC Championship umemalizika rasmi kwa KenGold kutawazwa mabingwa wa Ligi hiyo ikifikisha jumla ya alama 70 kwenye michezo 30 ikishinda 21, ikipata sare michezo 7 na kufungwa michezo 2.
Pamba FC imefanikiwa kupanda Ligi Kuu ya NBC moja kwa moja baada ya kushinda mchezo wa leo na kufikisha jumla ya alama 67 ambazo haziwezi fikiwa na timu yeyote inayomfuatia.
Mbeya kwanza na Biashara United watacheza hatua ya mtoano kutafuta timu moja kutoka Ligi ya NBC Championship itakayocheza hatua ya mtoano na timu moja toka Ligi Kuu ya NBC na mshindi wa Jumla kushiriki Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2024/2025.
Timu kutoka Ligi Kuu ya NBC itakayocheza hatua ya mtoano dhidi ya timu ya Ligi ya NBC Championship ni timu itakayopoteza mchezo wa mtoano kati ya timu iliyoshika nafasi ya 13 na 14 ndani ya Ligi Kuu ya NBC.
Timu za Pan African ya Dar es salaam na Ruvu Shooting ya Iringa zimeshuka daraja moja kwa moja na mwakani zitashiriki First League msimu wa 2024/2025.