TIMU ya African Sports ya Tanga imefanikiwa kuwa bingwa wa Ligi ya First League msimu wa 2023/24 baada ya kuifunga Kiluvya ya Dar es Salaam bao 1-0.
African Sports imefanikiwa kutwaa ubingwa huo bila kupoteza mchezo wowote katika mashindano ya First League Nane Bora yaliyofanyika Tanga kwenye uwanja wa Mkwakwani.
African Sports imefanikiwa kupanda daraja hadi Ligi ya Championship ya NBC baada ya kushuka msimu uliopita kwa kupoteza mchezo wa mtoano dhidi ya TMA ya Arusha.
Timu ya Kiluvya iliyopoteza fainali imefanikiwa kuibuka mshindi wa pili na kupanda Ligi ya Championship ya NBC msimu wa 2024/25.
Timu za Malimao iliyoibuka mshindi wa tatu na Mwadui iliyokuwa mshindi wa nne zitacheza michezo ya mtoano na timu zilizopoteza michezo yake ya mtoano kwenye ligi ya Championship ya NBC ili kutafuta nafasi ya kucheza ligi ya Championship ya NBC msimu wa 2024/25.