YANGA BINGWA LIGI KUU YA NBC.

 

USHINDI wa mabao 3-1 dhidi ya Mtibwa Sugar umeipa timu ya Yanga ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2023/2024 baada ya kufikisha jumla ya alama 71 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yeyote .

Huu ni ubingwa wa tatu mfululizo wa Ligi Kuu ya NBC kwa Young Africans tangu msimu wa 2021/2022 hadi msimu huu wa 2023/2024.

Vita ya nafasi ya pili ndio inayoendelea kwasasa Kati ya Azam FC na Simba SC zikiwania kuungana na Yanga kwenye uwakilishi katika Ligi ya Mabingwa Afrika msimu ujao.

Azam ipo nafasi ya pili ikiwa na alama 60 baada ya michezo 27 huku Simba SC ikiwa nafasi ya tatu na alama 57 baada ya michezo 26.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *