ARAJIGA

ARAJIGA PILATO WA ‘DERBY’ YA KARIAKOO.

BODI ya Ligi Kuu Tanzania leo Februari 5, imetangaza orodha ya maofisa watakaosimamia mchezo wa ‘DERBY’ ya Kariakoo wakiwemo waamuzi wa mchezo huo, Ahmed Arajiga kutoka Manyara aliyeteuliwa kuwa mwamuzi wa kati akisaidiwa na Mohamed Mkono kutoka Tanga na Kassim Mpanga wa Dar es Salaam huku mwamuzi wa akiba akiwa ni Amina Kyando kutoka Morogoro.

Maofisa wengine walioteuliwa kusimamia mchezo huo ni Pamoja na Salim Singano Kamisaa wa Mchezo, Soud Abdi Mtathmini wa Waamuzi, Baraka Kizuguto Mratibu wa Mchezo, Jonas Kiwia Mratibu wa Mchezo Msaidizi, Karim Boimanda Afisa Habari, Fatma Abdallah Afisa Protokali, Jerry Temu Afisa Masoko, Manfred Limbanga Daktari wa mchezo, ASP Hashim Abdallah Afisa Usalama na Ramadhan Misiru Msimamizi wa Kituo.

Ni siku tatu pekee zimesalia kwenda kushuhudia mchezo huo mkubwa zaidi kwenye Ligi namba nne (4) kwa ubora barani Afrika.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *