Author: James Onesmo

WANAHABARI WATAKAOHUDHURIA SEMINA YA KUWAJENGEA UWEZO

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imeandaa Semina ya siku moja ya kuwajengea uwezo Wanahabari wanaoandika habari za michezo (hasa mpira wa miguu).

Semina hiyo itafanyika kuanzia saa 2:00 asubuhi Jumatatu Agosti 29, 2022 kwenye ukumbi wa mikutano uliopo ghorofa ya kwanza, Jengo la NSSF (Mafao House) lililopo Ilala Boma mkoani Dar es Salaam.

Ifuatayo ni orodha ya Wanahabari watakaohudhuria Semina hiyo ambayo itatanguliwa na zoezi la usajili na kupata kifungua kinywa kuanzia saa 1:00 asubuhi hadi saa 1:50 asubuhi;

Na JINA CHOMBO CHA HABARI
1 ABDALLAH HAMISI ZEZE INK MEDIA TZ
2 ABDUL MIKIDADI UHURU FM
3 ABDURAHMAN JUMANNE UHURU PUBLICATIONS LIMITED
4 ABUBAKARI MKOBA MUUNGWANA BLOG & TV
5 ABUU RAMADHANI ALLY AYUZA TV
6 ABUU RAMADHANI MWAKYOMA SUPA TV
7 ABUUBAKARI SAID WASAFI MEDIA
8 ALBERT MRINGO MPENJA TV
9 ALFA SIASA ASPORT TZ
10 ALFRED KAVISHE TBC
11 ALHAJI ZUBERI RAJABU MKULE TV
12 ALLY SUKEIMAN MZURI MZURI TV
13 ALUMANUS JULIUS MWASENGA YO! FAVE TV
14 AMANI JOVIN NDIMBO ACTIVE MEDIA
15 AMEDEUS VICTOR SOMI GANGANA INFO CHANNEL
16 AMINA YUSUPH CFM
17 ASHA KIGUNDULA TANZANIA LEO
18 BADI MCHOMOLO TIMES RADIO FM
19 BAKARI KAGOMA BOIPLUS TV
20 BARAKA SILVANUS KIDANI STARS
21 CHRISTIANI MALIBATE C SPORT MEDIA
22 CLECENCE KUNAMBI DAILY NEWS
23 CLEMENT JOHN HITS FM – ZANZIBAR
24 CLEZENCIA TRYPHONE MWANANCHI & MWANASPOTI
25 CLINTON EPIMACK JR MTITA TV
26 COSMASY CHOGA SPORTS STAR TZ
27 CYPRIAN EMMANUEL KASHETO TV3
28 DALIDALI RASHID CLOUDS MEDIA
29 DAMIAN DENIS THEOBALD CLASSIC FM
30 DAUDI YASSIN NABWERA NYIRO TV
31 DAUKA ABRAHAM SOMBA DAR24 MEDIA
32 DAVID NELSON SHIJA MZEE WA MIKITO
33 DAVID PASCHAL SIBUKA MEDIA LIMITED
34 DERICK DAVID KAHIMBA KABUMBU TV
35 DIANA JOHN SONGA BOIPLUS TV
36 DICKSON BISARE MOGENDI MATUKIO DAIMA TV
37 DICKSON R. MASANJA DAUDA TV (ONLINE)
38 DIDAS OLANG JFIVE TV ONLINE
39 DISMAS HILARY ACTIVE MEDIA
40 EDGAR JOHN KIBWANA CLOUDS MEDIA
41 ELISHA PIUS YOHANA REAL MEDIA
42 ELIZABETH JOHN UHURU MEDIA GROUP
43 EMESTO ELIUD SIMKWAI JFIVE MEDIA
44 ESTER FRANCK LEMA AYOMA TV
45 FADHILI OMARY SIZYA DIZZIM FM MOROGORO
46 FARHAN KIHAMU CLOUDS MEDIA
47 FARIDI MIRAJI TBC
48 FATUMA RASHID MBELWA PLUS RADIO
49 FELIX JASON SOKAONLINE
50 FRADIUS MUGOA TBC
51 FREDRICK NWAKA TBC
52 FURAHA RAJABU CHABRUMA JR MTITA TV
53 GERVAS MAKASI JOHN MPENJA TV
54 GIDEON NJONANJE BONA TV
55 GODFREY NYANTO TBC FM
56 GRACE MILANZI MAXIMUM TV
57 GRACE MKOJERA HABARILEO
58 HAJI N SAMRI CLOUDS MEDIA GROUP
59 HAMIS SELEMAN MAHURUKU HITS FM DAR ES SALAAM
60 HAMZA FUMO BONGO5 MEDIA GROUP LTD
61 HASSAN DAUDI DIMBANI
62 HONEST AMON MWANITEGA FREELANCER
63 HUMPHREY MSECHU SPARKLIGHT TV
64 HUSEIN MOHAMED GLOBAL TV
65 HUSEIN SHAFII TBC
66 HUSSEIN MIRAJI MCHOMVU LAXY TV
67 IBRAHIM LOITORE SIKON MWANANCHI & MWANASPOTI
68 IBRAHIM MUSSA GLOBAL PUBLISHERS
69 IBRAHIM THABIT SANGA SUPA TV
70 INNOCENT OKAMA TFF MEDIA
71 ISAACK WAKUGANDA MUST FM RADIO
72 ISIKE PETER FRED SUPA TV
73 ISMAIL HUSSEIN MWAMBA MWAMBAFIVE (ONLINE TV)
74 ISSA SALUMU LIPONDA GLOBAL PUBLISHERS
75 JACKSON SILLO ITV / RADIO ONE
76 JAMES ABLE BONA TV
77 JAMES JOSEPH RANGE TBC
78 JAMILLA KASSIMU WRM TV
79 JAPHARY LESSO LONGA TV
80 JOHN MACHELA MASHUJAA FM
81 JOHN MAGANGA TV3
82 JOHN RICHARD MARWA SIBUKA FM
83 JOSEPH BENEDICTOR KESSY TIMES FM RADIO
84 JOSEPH SOPOLA DAVID HABARI FM, ZANZIBAR LEO
85 JUMA BAKARI KINANGUKA ZENJ FM
86 JUMANNE MAKAMBI KINGO BOIPLUS TV
87 KALUNDE MAHIMBO SAID TBC
88 KHATIMU AHMEID NAHEKA MWANANCHI
89 KUSHOKA JOSEPH MISHPLUS TV
90 LATIFA MSABAHA TVE TANZANIA
91 LEONARD SYLVESTER NYONI STAR TV
92 MALYO CHETO NJEDENGWA TBC
93 MAREGES NYAMAKA REDIO FREE AFRICA
94 MARTHA MBOMA GLOBAL GROUP
95 MARTIN MAZUGWA HABARI LEO
96 MBWANA SHOMARI STAR TV
97 MEMORASIA SYLVESTER LAXY TV
98 MICHAEL NYANKONGO VALOR TV
99 MOHAMED AKIDA HABARI LEO
100 MOHAMMED ALLY BALHABOU KASI MEDIA
101 MOHAMMED MDOSE HABARI LEO (TSN)
102 MSHAMU HASSAN CLASSIC FM
103 MSHAMU NGOJWIKE WANANCHI SPOTI
104 MUHSINI ABU KIMONJE WALLENIVO MEDIA
105 MWINYIMVUA NZUKWI ZANZIBAR LEO/ZANZIBAR MAIL
106 NASRA KITANA UHURU PUBLICATIONS LIMITED
107 NASSIB MKOMWA ATHUMANI CLOUDS MEDIA
108 NAZARETH JOSEPH UPETE TBC
109 NICKSON SYLVANUS BONFACE AYOMA MEDIA
110 NOEL RUKANUGA FULL SHANGWE TV
111 OMARY MDOSE GLOBAL PUBLISHERS
112 OSCAR N NKEMBO MPENJA TV
113 PATRICK DERRICK MWANKALE AM24 RADIO
114 PATSON MWITA AMSHA MEDIA
115 PETER LUGENDO JOHN TBC FM
116 PETER LUSSE BM TV TANZANIA
117 PETER MAVALA MAVALA TV
118 PHILIP N NYITI CLOUDS MEDIA
119 POLYCARP CLAUDIO MKAI TV
120 QUDRA KAIZA QTV TANZANIA
121 RAHEL JAPHET PALLANGYO TSN LTD
122 RAMADHAN ELIAS MWANANCHI COMMUNICATIONS LIMITED
123 RAMADHANI KAEMBA HTM NEWS
124 RICHARD DEOGRATUS SOMBI MTANZANIA DIGITAL
125 ROBERT RICHARD AMGL
126 SAADA AKIDA IPP MEDIA – NIPASHE
127 SAID ALLY GLOBAL PUBLISHERS
128 SAID ALLY MWANDIKE WAPO RADIO FM
129 SALUM BAKARI KAORATA BM TV TANZANIA
130 SHUFAA LYIMO THE GUARDIAN
131 SILAS MBISE WAPO MEDIA
132 SIMON RUGEGERA MKAI TV
133 SOMOE NG’ITU THE GUARDIAN LIMITED
134 STANSLAUS LAMBAT DAR24 MEDIA
135 STELLA T KESSY LAJIJI
136 SUZANA MAKORONGO MATUKIO BLOG
137 TAGATO J TAGATO TV3
138 THOBIAS ROMMY CELEB AFRICA TV
139 THOMAS JULIUS MSELEMU KANDANDA
140 TIMA SALEHE SIKILO SHIRIKA LA MAGAZETI YA SERIKALI ZANZIBAR
141 TUMAINI ABISSAY STEPHEN EATV & EA RADIO
142 URUGHU SALUMU BWIGANE TV
143 VENANT MTAKINGILWA GLOBAL PUBLISHERS
144 VICTORIA MUNGURE WAPO MEDIA
145 WALTER EZRAEL SIBUKA FM
146 WASTARA KHERI MSESE KISS FM TANZANIA
147 YUSUPH KATALAMBULA MIKASA TELE
148 ZAINA MOHAMMEDY AYOMA ONLINE TV
149 ZAMOYONI MBWALE TUZO ONLINE
150 ZUBERI HEMEDI MAKUNGE KITENGE TV

LIGI KUU YA NBC MWENDO MDUNDO

Ligi Kuu ya NBC raundi ya pili imetamatika jana Agosti 21, 2022 kwa michezo minne kuchezwa na kukamilisha jumla ya michezo minane katika raundi ya pili.

Mchezo wa mapema ulizikutanisha Mtibwa Sugar na Ruvu Shooting saa 8:00 mchana katika uwanja wa Manungu, Turiani mkoani Morogoro na Mtibwa Sugar kushinda kwa mabao 2-1. Michezo miwili ya saa 10:00 ilizikutanisha Polisi Tanzania na KMC FC kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha ukimalizika kwa sare ya mabao 2-2 huku ule wa Singida Big Stars na Mbeya City ukimalizika kwa Singida kuibuka na Ushindi wa mabao 2-1.

Mchezo wa Azam FC dhidi ya Geita Gold uliochezwa kwenye uwanja wa Azam Complex majira ya saa 1:00 usiku ndio ulikuwa mchezo wa mwisho kwa raundi ya pili na kumalizika kwa sare ya bao moja.

Simba SC inaendelea kubaki kileleni ikiwa na alama sita ikifuatiwa na Yanga SC yenye alama sita, nafasi ya tatu inashikiliwa na Singida BS ikiwa na alama sita huku utofauti ukiwa katika mabao ya kufunga na kufungwa.

Mabao 20 yamefungwa  katika raundi ya pili na kufanya jumla ya mabao 40 yawe yamefungwa hadi sasa ndani ya msimu huu wa 2022/2023, Reliants Lusajo ndiye anayeongoza mbio za ufungaji akiwa amefunga mabao matatu akifuatiwa na Salum kipemba, Fiston Mayele, Matheo Anthony, Moses Phiri, Nassor Kiziwa, Sixtus Sabilo na Tepsie Evance wakiwa na mabao mawili kila mmoja.

Mpaka hivi sasa ni Ihefu SC pekee ndio ambao hawajafunga bao lolote huku Simba SC ikiwa ndio timu pekee ambayo haijaruhusu bao.

Ligi Kuu ya NBC imesimama hadi Septemba 6, 2022 kupisha mechi za timu ya taifa kuwania kufuzu michuano ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani.

MZUNGUKO WA PILI LIGI KUU YA NBC

Ligi Kuu ya NBC inaendelea hii leo kwa mchezo mmoja kuchezwa baina ya Ihefu SC na Namungo FC katika uwanja wa Uhuru kuanzia saa 10:00 alasiri.

Ihefu wanatumia uwanja wa Uhuru kama uwanja wao wa nyumbani baada ya uwanja wao wa Highland Estates kufungiwa kutokana na kutokidhi vigezo vya kikanuni na sheria za mpira wa miguu.

Wakiongea na waandishi wa habari kocha wa makipa na nahodha wa kikosi cha Namungo wamesema wapo tayari Kwenda kuwakabili Ihefu SC kwa kuwa wamejiandaa vya kutosha.

“Mchezo wa mwanzo ulikuwa mgumu lakini kwavile tushajua Ligi iko vipi tumejipanga vizuri kuhakikisha tunaondoka na alama tatu,” alisema Faruk Ramadhani Kocha wa makipa wa Namungo.

Wakati huo huo nahodha wa timu hiyo Reliants Lusajo alisema malengo waliyoyapanga msimu uliopita hayakufanikiwa lakini msimu huu wanaamini watafanya vizuri na kuweza kushika nafasi nne za juu.

Kocha na nahodha wa Ihefu SC walishindwa kutokea katika mkutano huo kutokana na kupata changamoto za usafiri wakiwa safarini kuja Dar es saalam.

Raundi ya pili itaendelea tena kesho Agosti 20,2022 kwa michezo mitatu, michezo miwili  ya mapema itazikutanisha Coastal Union na Yanga SC katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha wakati Dodoma Jiji wakiwakabili Tanzania Prisons kwenye uwanja wa Liti mkoani Singida kuanzia saa 10:00 alasiri.

Mchezo wa mwisho kesho utachezwa saa 1:00 usiku kati ya Simba SC na Kagera Sugar katika uwanja wa Benjamin Mkapa.A

KIVUMBI CHA LIGI KUU YA NBC KUANZA LEO

Pazia la Ligi kuu ya NBC msimu wa 2022/2023 linafunguliwa rasmi  hii leo Agosti 15, 2022 kwa timu nne za Ihefu SC, Ruvu Shooting FC, Namungo FC na Mtibwa Sugar FC  kushuka katika viwanja viwili kuzisaka alama tatu.

Mchezo wa kwanza wa ufunguzi utazikutanisha Ihefu  dhidi ya Ruvu Shooting majira ya saa 10:00 alasiri katika dimba la Highland Estate, Mbarali  Mkoani Mbeya wakati mchezo wa pili utazikutanisha  Namungo dhidi ya Mtibwa Sugar katika dimba la Benjamin Mkapa kuanzia saa 1:00 usiku.

Timu ya Namungo  inatumia uwanja wa Benjamin Mkapa kama uwanja wake wa nyumbani baada ya uwanja wao wa Majaliwa, Lindi kuwa  katika maboresho.

Msimu huu wa 2022/2023 unashirikisha jumla ya timu 16 ambapo kila timu itacheza jumla ya michezo 30 kwa mtindo wa nyumbani na ugenini na  kufanya jumla ya  michezo 240 sawa na michezo 120 nyumbani na 120 ugenini kwa timu zote.

KLABU, TFF, TPLB KUNUFAIKA NA MAFUNZO YA UEFA ASSIST

Tanzania imepata bahati ya kufikiwa na Programu ya UEFA ya Maendeleo ya Mpira wa Miguu (UEFA Assist) ambapo imeandaliwa semina maalum yenye lengo la kuboresha Ligi za Tanzania na Uendeshaji wa Mashindano nchini.

Programu hiyo ilianza Novemba 2021 kwa zoezi la kukusanya maoni ya wadau mbalimbali wakiwemo makocha, wachezaji, Wanahabari, viongozi wa Shirikisho na Bodi ya Ligi, viongozi wa klabu, wadhamini na washabiki.

Hatua ya pili ya Programu hiyo ni semina ambayo itaendeshwa na maafisa wa UEFA Assist kwenye hoteli ya Golden Tulip mkoani Dar es salaam kuanzia Januari 10 hadi 15, 2022.

Washiriki wa semina hiyo ni viongozi na maafisa wa TFF na Bodi ya Ligi, viongozi na maafisa wa klabu za Ligi Kuu (Mwenyekiti/Rais, Katibu/CEO, Mkurugenzi wa Ufundi na Afisa wa Fedha na Mipango).

Baada ya semina hiyo, Programu itaingia katika hatua ya tatu ambapo maafisa wa UEFA Assist watasimamia utekelezaji wa mapendekezo ya maboresho Ligi na Uendeshaji wa Mashindano nchini.