DODOMA YAPANDA NAFASI YA SITA LIGI KUU YA NBC.

 

DODOMA Jiji imeendelea kuonyesha makali yake kwenye Ligi Kuu ya NBC baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2–1 dhidi ya KMC katika mchezo uliochezwa Jijini Dodoma kwenye uwanja wa Jamhuri.

Bao la kwanza la Dodoma Jiji lilifungwa dakika ya 43 na Faraji Kayanda na Kipindi cha kwanza kumalizika Dodoma ikiwa mbele kwa bao moja.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku KMC ikijaribu kusawazisha na jitihada zao zilifanikiwa dakika ya 76 baada ya Rashid Chambo kufunga bao la kusawazisha na kuirejesha timu yake mchezoni.

Hata hivyo iliwachukua dakika moja pekee Dodoma kurejea kwenye uongozi kwa bao la Iddi Kipangwile na kufanya mabao kuwa 2–1 hadi mchezo unamalizika.

Katika mchezo huo, Khleffin Hamdoun alionyesha kiwango cha juu na hatimaye kuchaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa Mechi akichangia kwa kiasi kikubwa ushindi wa Dodoma Jiji.

Ushindi huo unaifanya Dodoma Jiji kufikisha alama 17 na kuendelea kushika nafasi ya sita kwenye msimamo wa ligi huku KMC ikisalia nafasi ya mwisho (16) ikiwa na alama 8 hali inayozidi kuwaweka kwenye presha ya kusaka matokeo chanya katika michezo ijayo ili kusalia Ligi Kuu ya NBC.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *