FIRST LEAGUE KUHITIMISHWA LEO.

FIRST LEAGUE KUHITIMISHWA LEO.

LIGI ya First League inahitimishwa leo kwa michezo ya Kundi A na B kwa timu zote kundi A na timu sita kundi B kutupa karata zake kuanzia saa 10:00 jioni,

Tayari timu ya Hausung ya mkoani Njombe imeshakata tiketi ya moja kwa moja  kushiriki Ligi ya championship ya NBC msimu wa 2024/2025 kutoka kundi A huku ikisubiriwa timu ya kupanda moja kwa moja kutoka kundi B ambapo timu za Rhino Rangers, Gunners, na Tanesco zina nafasi kubwa ya kufanya hivyo.

Ikumbukwe kuwa timu inayoshika nafasi ya kwanza kwenye msimamo wa First League Kundi A na B Inafuzu moja kwa moja kushiriki Ligi ya Championship ya NBC.

Wakati timu zinazoshika nafasi ya pili na ya tatu kwenye kila kundi zikicheza michezo ya mtoano (PlayOff) kupata washindi wawili wa kucheza mtoano wa kupanda (Promotion PlayOff) na timu mbili za ligi ya Championship ya NBC.

 

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *