FOUNTAIN GATE YAJIPATA,MASHUJAA MAMBO MAGUMU

LIGI Kuu ya NBC jana michezo iliendelea kwa michezo mitatu iliyochezwa mikoa mitatu tofauti Manyara,Singida na Kagera.

Fountain Gate iliwakaribisha timu ya Tanzania Prisons katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa mchezo uliochezwa majira ya saa nane mchana.

Dakika ya 27  Fountain Gate walipata bao kupitia mchezaji wao Amos Kadikilo kwa mkwaju wa penati na ambalo ndio bao pekee katika mchezo huo na lilipelekea timu hiyo kuvuna alama zote tatu na kufikisha alama 25 nafasi ya nane ya katika msimamo wa Ligi Kuu.

Mchezaji wa Fountain Gate Amos Kadikilo alitangazwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo dhidi ya timu ya Tanzania Prisons ambayo ipo nafasi ya 14 ikiwa na alama 18.

Singida Black Stars iliwaalika Mashujaa majira ya saa kumi alasiri uwanjani CCM Liti, mchezo ulianza kwa kasi na timu zote zilishambuliana kwa kasi hadi kufikia mapumziko hakuna aliyeona lango la mwenzake.

Kipindi cha pili kilianza ambapo dakika ya 57 mshambuliaji wa Singida,Jonathan Sowah alifungua ukurasa wa mabao kupitia mkwaju wa penati na dakika ya 60 aliongezea bao la pili huku Elvis Rupia akiongeza bao la tatu dakika ya 90 ya mchezo huo ambao uliisha kwa ubao kusomeka 3-0.

Mshambuliaji wa Singida Black Stars, Jonathan Sowah alitangazwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo akiisaidia timu yake kufikisha alama 41 wakiwa nafasi  ya nne katika msimamo wa Ligi Kuu huku Mashujaa wakiwa nafasi ya 11 na wakivuna alama 23.

Mchezo wa mwisho ni Kager Sugar iliwakaribisha timu ya KMC majira ya saa moja jioni katika uwanja wa Kaitaba.

Mchezo ulikuwa wa kasi ambapo timu zote mbili zilikuwa zikishambuliana kwa kasi jambo lililopelekea mcheo huo kumalizika kwa 0-0 na mchezaji wa Kagera Sugar,Eric Mwijage atichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.Kagera walifikisha alama 16 wakiwa nafasi ya 15 huku KMC wakiwa nafasi ya 10 na alama 24.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *