JKT YASHINDWA KUTAMBA NYUMBANI LIGI KUU YA NBC.

TIMU ya JKT Tanzania yenye ‘maskani’ yake uwanja wa Isamuhyo, Dar es Salaam imeshindwa kutamba kwenye uwanja wake wa nyumbani baada ya kulazimishwa sare ya 2-2 na timu ya Dodoma Jiji.

Pamoja na kutangulia kupata bao kupitia kwa nahodha wake Edward Songo JKT ilishindwa kuizuia Dodoma iliyokuwa ikifanya mashambulizi ya mara kwa mara na kusawazisha mara zote JKT ilipotangulia kwa uongozi.

Mwana Kibuta aliinyima JKT uongozi hadi mapumziko baada ya kusawazisha bao la Songo zikiwa zimesalia sekunde chache kabla ya mapumziko.

Songo aliongeza bao la pili dakika ya 66 na kuipa JKT uongozi uliodumu kwa dakika 15 pekee kabla ya Paul Peter kuisawazishia Dodoma Jiji na kufanya matokeo kuwa 2-2 hadi mwisho wa mchezo.

Matokeo hayo yanaifanya JKT kushika nafasi ya sita na kuwa mbele ya Dodoma inayoshika nafasi ya saba kwa tofauti ya alama tatu.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *