JKT,KEN GOLD HAPATOSHI LEO LIGI KUU YA NBC

LIGI Kuu ya NBC inaendelea kwa michezo miwili inayopigwa mkoani Dar es salaam katika viwanja vya Meja Jenerali Isamuhyo na Azam Complex.

JKT Tanzania wazee wa ‘kichapo cha kizalendo’ itawakaribisha Ken Gold ‘wazee wa makarasha’ katika mchezo utakaochezwa saa kumi alasiri.

Ikumbukwe kuwa JKT Tanzania ipo nafasi ya sita kwenye msimamo ikiwa imefunga mabao 15 ikiruhusu mabao 15 na kukusanya alama 26 katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

Kwa upande wa Ken Gold ipo nafasi 16 ikiwa imefunga mabao 17 ikiruhusu 37  ikiwa imekusanya alama 14 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

Mchezo wa pili utachezwa Azam Complex uliopo Chamazi Dar es Salaam majira ya saa moja usiku ambapo timu ya Azam itawakaribisha Namungo.

Azam ipo nafasi ya tatu katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa imefunga mabao 31 ikiruhusu mabao 11 na  ikikusanya alama 44 .

Namungo ipo nafasi ya 13 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa imefunga mabao 15 ikiruhusu mabao 26 na kukusanya alama 22.

 

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *