KMC, COASTAL ZATAMBA LIGI KUU YA NBC

LIGI Kuu ya NBC msimu wa 2025/2026 imefunguliwa kwa michezo iliyochezwa kwenye viwanja vya KMC Complex mkoani Dar es salaam na Mkwakwani, Tanga na kushuhudia KMC na Coastal Union zikitamba kwa ushindi nyumbani.

Goli pekee la ushindi la KMC lilifungwa na Daruweshi Saliboko dakika ya 56 kipindi cha pili baada ya kipindi cha kwanza kumalizika kwa sare ya bila kufungana.

DARUESHI SALIBOKO - KMC
DARUESHI SALIBOKO – KMC

KMC wamekusanya alama zao tatu za kwanza za msimu wa 2025/26 na kuwa timu ya kwanza kushinda mchezo huku Daruweshi Saliboko akiwa mfungaji wa bao la kwanza la msimu.

Mchezo wa pili ulichezwa mkoani Tanga majira ya saa moja kamili jioni uwanja wa mkwakwani ambapo Coastal union waliwakaribisha Tanzania Prisons.

Kipindi cha kwanza kilitosha kwa Coastal kujihakikishia alama zake tatu kwa bao la kiungo wa zamani wa Azam na Dodoma Jiji Cleophace Mkandala lililodumu hadi mwisho wa mchezo.

Matokeo hayo yanaifanya Coastal union kuungana na KMC na kuwa timu za kwanza kukusanya alama tatu kwenye Ligi Kuu ya NBC msimu huu.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *