LADHA ZA LIGI KUU KUCHEZWA VIWANJA VITATU

LIGI Kuu ya NBC itaendelea leo kwa mzunguko wa 22  kuanza kuchezwa  katika viwanja vitatu tofauti nchini kuanzia saa nane mchana.

Mchezo wa kwanza utakaochezwa leo saa nane mchana ni timu ya Fountain Gate itaikaribisha timu ya Tanzania Prisons katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa mkoani Manyara majira ya saa nane mchana.

Fountain Gate ipo nafasi ya 13 kwenye msimamo wa Ligi Kuu huku  ikiwa imevuna alama 22 na kufunga mabao 25 na kufugwa 39 na Tanzania Prisons ipo nafasi ya 14 ikiwa na alama 18 mabao y kufunga 12 na kufungwa 26.

Singida Black Stars itaikaribisha timu ya Mashujaa katika uwanja wa CCM Liti mkoani Singida mchezo utakaochezwa majira ya saa kumi jioni.

Singida Black Stars ipo nafasi ya nne katika msimamo wa Ligi Kuu ikiwa imefunga mabao 28 na kuruhusu nyavu zao kufungwa mara 19, Mashujaa ipo nafasi ya tisa katika msimamo ikiwa imefunga mabao 17 na kufunwa mabao 23.

Mechi ya mwisho leo itachezwa majira ya saa moja jioni ambapo timu ya Kagera Sugar itaikaribisha timu ya KMC katika uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera.

Kagera Sugar ipo nafasi ya 15 kwenye msimamo ikiwa imefunga mabao 16 na kuruhusu mabao 30 huku KMC ikiwa nafasi ya 10 ikiwa na alama 23 na ikifunga mabao 15 na kuruhusu 32.

 

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *