LIGI KUU YA NBC

LIGI KUU YA NBC KUCHEZWA VIWANJA VINNE LEO.

LIGI Kuu ya NBC inaendelea kwa mzunguko wa 17 huku mechi nne zikichezwa katika viwanja mbalimbali nchini kuanzia majira ya saa nane mchana.

Mchezo wa kwanza utachezwa saa nane mchana katika  uwanja wa Jamhuri Dodoma ambapo Dodoma Jiji watawakaribisha Pamba Jiji kutoka jijini Mwanza .

Sambamba na mchezo huo Tanzania Prisons “wajelajela” watawakaribisha timu ya Mashujaa “Wana mapigo na mwendo” katika uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya  muda ikiwa ni saa nane mchana.

Mchezo  wa tatu  kwa siku ya leo ni timu ya Fountain Gate watawakaribisha  timu ya Simba katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa uliopo Babati Mkoani Manyara saa kumi alasiri.

Mkoani Dar es Salaam wenyeji wa  uwanja wa Chamazi  timu ya Azam watawakaribisha timu ya KMC “Kinoboys” katika mchezo utakaochezwa saa moja jioni.

 

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *