LIGI ya NBC Championship inaendelea hii leo kwa michezo mitatu kupigwa huku yote ikionyeshwa mubashara kupitia TV3.
Mapema saa 8:00 Mchana Stand united itaikaribisha Mbuni kwenye uwanja wa Mwadui Complex mkoani Shinyanga.
Mkoani Mtwara Mbeya kwanza itakuwa mwenyeji wa FGA talents kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona saa 10:00 alasiri na kuoneshwa Live kupitia ST BONGO
Mchezo wa mwisho utapigwa Saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Mabatini mkoani Pwani ambapo Pan Africans itakuwa mwenyeji wa Pamba.
Hii ndio michezo ya mwisho kukamilisha mzunguko wa 17 wa Ligi ya NBC Championship.