NBC CHAMPIONSHIP KINAWAKA LEO.

 

LIGI ya NBC ya Championship mzunguko wa Nne unaanza Leo kwa michezo mitatu kuchezwa kwenye mikoa ya Mtwara, Arusha na Morogoro.

Mkoani Mtwara Mbeya Kwanza itakuwa mwenyeji wa Green Warriors kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona kuanzia saa 8:00 Mchana.

Mbuni FC ya Arusha itaialika Biashara United ya Mara kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha kuanzia saa 10:00 alasiri.

Mchezo wa mwisho kwa leo utazikutanisha Mtibwa Sugar dhidi ya Songea United kuanzia saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Manungu mkoani Morogoro.

Hadi hivi sasa Mtibwa Sugar inaongoza msimamo wa Ligi ya NBC ya Championship ikiwa na alama tisa sawa na Songea United na Stand United zikitofautiana magoli ya kufunga na kufungwa.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *