BAADA ya KMC kupata ushindi wa kwanza wa Ligi Kuu ya NBC jana dhidi ya KenGold kwa bao moja huku Kagera Sugar ikitoka suluhu na JKT Tanzania leo ligi hiyo inaendelea kwa michezo miwili.
Mapema saa 8:00 mchana timu ya Pamba ya Mwanza itakuwa mwenyeji wa Singida BS kwenye uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.
Pamba haijaruhusu bao mpaka sasa huku ikitoa suluhu kwenye michezo yake mitatu iliyocheza dhidi ya Prisons, Dodoma Jiji na Azam FC huku timu ya Singida ikishinda michezo yote mitatu iliyocheza na KenGold, Kagera Sugar na KMC.
Saa 10:15 alasiri Coastal Union ambayo haijapata ushindi wowote msimu huu itakuwa uwanja wa nyumbani Azam Complex dhidi ya Namungo iliyopoteza michezo yote ya Ligi Kuu ya NBC hadi sasa.