LIGI Kuu ya NBC imeendelea kwa mchezo mmoja ambapo Namungo walikuwa wenyeji wakiikaribisha Simba katika mchezo uliochezwa majira ya saa kumi jioni katika uwanja wa Majaliwa mkoani Lindi.
Mchezo huo ulimalizika kwa Simba kupata ushidi wa mabao 3-1 huku wakionyesha ubora wao hasa katika kipindi cha kwanza walipofanikiwa kupata bao la mapema kupitia kwa Libasse Gueye dakika ya 12 kabla ya kuongeza bao la pili kupitia kwa Anicet Oura dakika ya 25.
Namungo walijaribu kurejea mchezoni na kufanikiwa kupata bao lao dakika ya 33 kupitia Haritier Makambo aliyefunga kwa mkwaju wa penati lakini juhudi zao hazikutosha kuizuia timu ya Simba.
Kipindi cha pili Simba waliendelea kuwa hodari kwenye mchezo huo mbele ya mashabiki wao wa mkoa wa Lindi na kuongeza bao la tatu dakika ya 74 kupitia Elie Mpanzu aliyehitimisha ushindi huo Muhimu kwa ‘Mnyama’.
Ushindi huo unaifanya Simba kuwa na alama 42 ikishika nafasi ya pili huku Namungo wakiwa nafasi ya 10 na alama 22.
Katika mchezo huo winga wa Simba Anicet Oura alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.