LIGI Kuu ya NBC imeendelea leo Februari 13, 2025 kwa mchezo mmoja kwenye uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, ukizikutanisha JKT Tanzania dhidi ya Singida Black Stars na kumalizika kwa Singida kushinda kwa bao 1.
Bao pekee la Singida Black Stars hii leo limefungwa na Jonathan Sowah dakika ya 52 ya mchezo akimalizia kazı iliyofanywa na Arthur Bada.
Kwa ushindi huo Singida Black Stars inaendelea kusalia nafasi ya 4 kwenye msimamo ikifikisha alama 37 baada ya michezo 19.
Katika hatua nyengine mchezaji Jonathan Sowah amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo kutokana na mchango wake mkubwa kwa timu yake kuondoka na alama tatu akifunga bao pekee na la ushindi kwa Black Stars.