MZUNGUKO wa 28 unatarajiwa kukamilika leo kwa mchezo mmoja utakaozikutanisha timu za Tabora United kutoka mkoani Tabora dhidi ya KMC ya Dar es Salaam saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora.
KMC itashuka ugenini ikiwa na kumbukumbu mbaya ya kupoteza mchezo wake uliopita dhidi ya Simba kwa mabao 1-2 kwenye uwanja wake wa nyumbani.
Hadi sasa ikicheza viwanja vya ugenini KMC imeshinda mchezo mmoja pekee, kufungwa michezo saba huku ikitoka sare minne na kukusanya alama saba pekee.
Tabora inashuka uwanjani ikiwa haijafanikiwa kupata ushindi kwenye michezo mitano mfululizo ya Ligi Kuu ya NBC na mara ya mwisho kushinda ilikuwa kwenye mchezo dhidi ya Dodoma Jiji kwa bao moja lililofungwa na Offen Chikola kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora.
 
					